✍️SOMO✍️PETE YA NDOA. - EDUSPORTSTZ

Latest

✍️SOMO✍️PETE YA NDOA.


Nawasalimu Watumishi Wa Bwana Katika jina la Yesu Inawezekana ndio Mara ya Kwanza kujiunga Ukurasa huu wa Moto wa Yesu Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa Nakukaribisha kujua historia ya Pete ya ndoa
Wengi Tunavaa Pete huwa bado hatuelewi Pete ya ndoa ilianzia wapi na kwanini unapofungishwa ndoa unavishwa Pete hususa kwa wakristo wote.
Tufunue Biblia Zetu Tusome;Kutoka;26;29 Luka;15;22-32 Yakobo;2:2-7 Mwanzo;38;18 isaya;3;20-22
✍️✍️Lengo la SoMo;Tujue Pete za ndoa umhimu wake na historia Yake.
✍️✍️DHIMA YETU MOTO WA YESU: Tujue kweli na kweli ituweke huru.
✍️✍️HISTORIA YA PETE YA NDOA✍️✍️
Pete ya ndoa iliazishwa kuvaliwa na Watu wa Agano la kale katika Falme mbalimbali wakati huo Pete ilikuwa ikivaliwa mkononi kumtambulisha mtu Kama Ni mtawala na mwenye Amri juu ya kitu fulani. Pete hii katika Agano jipya Tunaona Anavishwa mwana mpotevu ikiwa ishara ya kumtambulisha Mwanae kuwa Tena kuwa SI Mtoto aliyekosana na Baba Yake kwa upendo baba Anaamua aangize Aletewe Pete ambayo itambulishe upendo alionao baba mfano wa Pete Luka:15;22-32
Pete ilianza kuvaliwa miaka 3000 iliyopita Kutoka Kwenye kuvaliwa Pete na watawala Pete hii ilianza kuvaliwa na wanandoa na hii siyo angizo la Mungu wa Roho MTAKATIFU.
Isipokuwa Ni Mapokeo tuliopokea Kutoka Romani ilianzisha watu wavae Pete ikiwa na Lengo la Kuweka muunganiko kwa ishara ya Pete Kati ya mwanamke na MWANAUME
Tulipokea hivyo nasi Tunatembea katika utaratibu huo Katika Mapokeo hayo Kutoka Romani mpaka makanisa yote ya kikristo ishara Kubwa ya Mtu aliye Kwenye ndoa Ni Pete.
✍️✍️✍️ANGALIZO KWAKO✍️✍️
Sio kwamba upendo wa kweli upo Kwenye Pete hapana upo moyoni.
Sio kwamba mtu akivishwa Pete hatazini Kama mtu anasifa ya kuzini ataendelea tu
Sio Kwamba Pete ndio ndoa hapana ndoa Ni patano lenu Wawili mlilopatana
✍️✍️UMHIMU WA KUVAA PETE ya Ndoa✍️✍️
1;Pete hukujulisha kwa watu Kama wewe unakutana na watu wengi kuwa upo double sio single
2;Huwa inamtambulisha mtu na kumuweka aheshimi




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz