BADO UNAJIITA MWANAUME WAKATI UNA TABIA HIZI - EDUSPORTSTZ

Latest

BADO UNAJIITA MWANAUME WAKATI UNA TABIA HIZI

Na bado Unajiita mwanaume....
1. Umempa mimba mara tatu mwanamke wako, mara zote umemshinikiza azitoe halafu unamuacha, unaenda kuoa mwanamke mwingine. Halafu bado unajiita mwanaume.
2. Unamnyanyasa na kumpiga mkeo, unamdahrau mbele ya vinuka mkojo vyako. Halafu bado unajiita mwanaume.
3. Unambaka mwanamke na unadai unampenda sana. Halafu bado unajiita mwanaume.
4. Unalala na binti yako, eti kwa sababu umeona kifua kimechanua. Halafu bado unajiita mwanaume.
5. Una nyumba mbili na wake wawili. Na hakuna hata mmoja kati yao anaejua uko na mwanamke mwingine wa tatu. Na bado unajiita mwanaume.
6. Umepokea mshahara wako, unatumia kwenye pombe, sigara, wanawake na huachi kitu kwa mkeo. Na bado unajiita mwanaume.
7. Unaingia katika mahusiano, kwa ajili tu ya kumtumia huyo msichana kumkomoa mwanamke uliyekua unampenda. Na bado unajiita mwanaume.
8. Unamlazimisha mwanamke ngono kwa kutumia mamlaka yako aitha kielimu, kisiasa, kidini na pesa ulizonazo. Na bado unajiita mwanaume.
9. Unafanya ngono na mdogo wa mke wako, na unamwambia unatamani ungemuoa yeye. Na sasa ana ujauzito wako. Halafu bado unajiita mwanaume.
10. Unatembea huku suruali ipo katikati ya makalio, unatembea unanesa kama umekatika centre bolt, unatembea na selfie stick, uandishi wako ni wa 'Xaxa', 'xoxo', 'K' , unaongea huku unajiramba midomo na kurembua macho,Halafu unajiita mwanaume.
Ninao wasiwasi na uanaume wako, huenda ni mvulana....




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz