Sababu Za Kwanini Wanaume Huumia Zaidi Wanaposalitiwa Kimapenzi Zipo Hapa. - EDUSPORTSTZ

Latest

Sababu Za Kwanini Wanaume Huumia Zaidi Wanaposalitiwa Kimapenzi Zipo Hapa.

Sababu Za Kwanini Wanaume Huumia Zaidi Wanaposalitiwa Kimapenzi ...
Na wala hii haikufanyi usiwe wewe ulivyokuwa juzi. Amka watafute watu waambie ni jinsi gani umeumia, toa machungu yote ya nafsini mwako,inatokea kwa watu wengi Na wewe sio wa kwanza na wala sio wa mwisho.
Usiamini kupita kiasi
Mapenzi hayazuiliki ni kitu kinachokuja na kufunika moyo wako bila taarifa sio rahisi kucontrol mapenzi juu ya mtu fulani. Lakini unaweza kucontrol kumuamini mtu mwingine. Katika dunia tuliyonayo ni nadra kupata mtu mwenye mapenzi ya dhati,usimuamini sana amini kuWa ni tabia ya wanadamu kuchoka Na kutafuta vilivyo bora zaidi. Sisemi usiamini ila siku zote amini lolote linaweza kutokea itakusaidia siku ikiwa ndivyo sivyo.
Kusalitiwa hakuondoi thamani na utu wako
Baada ya kumfanyia yote uliodhani unamfanyia ili aendelee kukupenda lakini ameondoka, roho inakuuma sababu unaona hakumbuki jinsi gani ulivyojitoa kuhakikisha ana furahi na kuwa na amani siku zote. ii haiondoi ile asili na thamani ya utu wako maisha. Ni vile tu huna habari ila yamewakuta wengi na yataendelea. Kwanini wewe uone sio mtu tena, kwanini uone labda wewe sio mwanaume tena? Kwanini uone eti pengine uanamme wako una walakini Na sio yeye ndo mjinga kwa kutojua thamani ya penzi lako.
Amini anayekuja ni bora kuliko aliyeondoka
Ambacho hukijui ni kuWa kuna wanawake mamia kwa mamia wanasubiri mwanaume wa dizaini yako atokee ili kukamilisha maisha yao. Na ni bora kuliko aliyeondoka na watathamini mapenzi yako kuliko aliyekutenda. Jipe sababu ya kuamini wewe ni kama dini lililokuwepo enzi za babu zetu likichezewa bao mpaka mkoloni alipokuja kuwaonyesha thamani na matumizi sahihi ya madini!
Hautakiwi uache kupenda, hautakiwi upunguze juhudi za kumuonyesha mtu kama unampenda. Haijalishi ni mara ngapi unaumizwa unapofanya mazuri kwa mtu fulani usitegemee kitu hicho hicho kutoka kwa huyo mtu ila amini ni hazina uliyojiwekea na kuna siku utapata thamani ya penzi uliloliwekeza.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz