KAMA HUONI TOFAUTI YA KUWA MPWEKE NA YEYE KUWEPO USILAZIMISHE TENA MAPENZI KWAKE. - EDUSPORTSTZ

Latest

KAMA HUONI TOFAUTI YA KUWA MPWEKE NA YEYE KUWEPO USILAZIMISHE TENA MAPENZI KWAKE.

Image may contain: 2 people, outdoor

Usijiweke kwenye UPWEKE kwa kulazimisha Mtu awe wako wakati kwa MATENDO ni dhahili hakuhitaji, Umebaki kulazimisha PENZI ambalo halina uhai wowote wala hakuna MATUMAINI ya lini utakombolewa kwenye lindi la MAPITO UPITAYO😭
Kila ulipojaribu kutaka kujinasua alipojua alikubembeleza na kukusihi USIONDOKE
Lakini alipoona umetulia aliendelea na tabia yake ambayo ndiyo ilikupa wakati MGUMU😭😭
Kuacha afanyayo yakakuumiza hayupo tayari, Lakini pia kukuacha anahisi MOYO WAKE UTAUMIA😎
Maana yake anajua uwepo wako ni muhimu kwake lakini HAPENDI UWE NA AMANI mwisho wa yote ni wewe kubakia MPWEKE na mwingi wa MAWAZO
Hakupendi huyo wala hana MALENGO na wewe zaidi anakutumia kuwa AMANI ya moyo wake ili yeye aendelee na yale anadhani kwake yana maana kuliko kukupa AMANI kwa malipo ya AMANI unayompa
Ni ngumu mno Mtu asiyejua MAUMIVU ya mwenzie KUTHAMINI UPWEKE wako hivyo ni wakati kujisahihisha kwa UDHAIFU ulio nao juu yake na baada ya hapo CHUKUWA HATUA KUINUSURU NAFSI YAKO
Bila kujua MAPITO YAKO Huwezi kujua MUDA unaopoteza kwa mtu asiyekupenda, Wala huwezi kujua NGUVU KAZI uipotezayo kwenye penzi la MTU ASOJUWA THAMANI YAKO
Inuka ujitetee usingoje kununua kifurushi ili ukasome Maandiko ya akina #Elista_Kasema_ila_Sio_sheria Kwani hayo yanabaki kuwa maneno ya kuiboost akili yako tu lakini mwenye MAAMUZI NI WEWE.
#Elista_Kasema_ila_Sio_She
ria ðŸ”¨




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz