JE UNAIJUA THAMANI YA PENZI ULILOPO🤷🏽‍♂ - EDUSPORTSTZ

Latest

JE UNAIJUA THAMANI YA PENZI ULILOPO🤷🏽‍♂

Image may contain: one or more people and people sitting
Huwezi kuudananya MOYO wako kutompenda MTU AMBAYE YEYE NDIYE ALIYEKO KWENYE KUTA ZA MOYO WAKO
Hakuna aliye mkamilifu but twaweza kusahihishana na kuendelea mwisho wa siku wapo ambao watatamani JINSI MLIVYOWEZA KUULINDA UPENDO WENU... Lakini nikukumbushe UZINZI hauvuliki hata MUNGU anakubari kuachana ikiwa umegundua kwa uhakika mwenza wako ANAKUSALITI hapo wala usisome ushauri wangu JUST KUSEPAAAA😅Ukiwa unampenda Mtu na Unadhani yeye ndiye akupaye FARAJA Basi jiulize mara mbili mbili wakati unataka kuondoka kwake, Thamani ya UPENDO inatajwa kwa mambo mawili yanayotegemeana nayo ni;
FURAHA💃
AMANI✌🏼
Ukiyakosa hayo na Uko na Mtu usijidanganye kwamba iko siku utayapata, Maana uwapo na mahusiano na ukabaini kwamba UNAPEWA FURAHA NA AMANI hapo ndipo unatakiwa upashike na kupalinda kwa nguvu zako zote💪🏽
Ni rahisi akili kuweka ugomvi baina yake na Moyo, Kwani huo ndo ubin adam, Maana akili huogopa kwa kuhisi lakini Moyo huogopa kwa matendo, ndo maana palipo na pendo la kweli HUITUPA NJE HOFU! lakini ukiishajua ya kwamba UNAMPENDA usijaribu kumpuuza mwenza wako kwa makosa madogo madogo ambayo mngeyaongea nae akakuelewa mkamaliza tofauti zenu MNGELIPONYA PENDO LENU.
Ni rahisi kudhani kwamba akiondoka yupo ambaye atakuja na kumzidi yeye, Rafiki yangu waswahili waliposema "KIPENDA ROHO HULA NYAMA MBICHI" Walimaanisha kwamba NI NGUMU KULA KITU KIBICHI KAMA HUJAAMUA💃
Uliyempenda haji kama KIVULI bali alikuwepo kwa wajihi wake, Ukimpoteza uliyempenda kwa DHATI naomba ujue athali zake;
KUTOPENDA TENA.
KUKOSA FURAHA.
KUWA MPWEKE.
KUTOHISI MAPENZI.
KUJAWA NA HASIRA.
Na mengineyo mengi ambayo yanagusa UTASHI WA NAFSI NA MOYO💘
Ni kweli yapo mambo ambayo hubomoa penzi na kusababisha kuleta hasira kwenye akili na baadaye MOYO kuhisi unaonewa ila naomba ujue jambo moja KUIMALIZIA SAFARI NI BORA SANA hata kama unahisi ina njia mbovu, kuliko kurudi ulikotoka na KUIANZA UPYA SAFARI🤣🤣🤣🤣
Uliyenaye uliishajua madhaifu yake, Uliishajua namna ya kuishi nae, unajua awapo kawaida na awapo vibaya INATOSHA SANA KUWA NAE kikubwa unachitakiwa kukiona kwake ANAKUPENDA NA KUKUJARI💃 Kwani najua utakuwa mwenye Furaha na Amani, Unataka nini zaidi ya hayo?
Labda tukukusanyie chawa junia moja tukupatie ukaishi nao😂




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz