HII NI YAKO WEWE DADA ULIYEKO KWENYE MAHUSIANO AU NDOA INAKUHUSU ...! - EDUSPORTSTZ

Latest

HII NI YAKO WEWE DADA ULIYEKO KWENYE MAHUSIANO AU NDOA INAKUHUSU ...!

Image result for housegirl kicheche

Dada yangu, kama umeolewa au upo kwenye mahusiano siriasi na mwanaume ambaye mna mipango mingi. Humsaliti lakini una rafiki yako wa kiume ambaye mnaweza kuchart kwenye simu kwa njia ya SMS kwa zaidi ya lisaa lizima, mnapiga umbea tu kwa kuchart tena si mambo ya mapenzi mambo ya kawaida tu. Lakini rafiki huyo huyo, badala ya kukupigia simu anakupigia Video Call, narudia kama unarafiki yako wa kiume ambaye mmezoeana mpaka imefikia hatua anakupigia Video Call basi jua kuwa unakaribia kuvunja ndoa au mahusiano yako.
Naomba nirudie, kama una mwanaume ni rafiki yako, mna mazoea mpaka mnaweza kuchart kwa meseji kwa zaidi ya lisaa lizima mnapiga umbea, lakini kama una mwanaume ni rafiki tu lakini mara kwa mara mnapigiana Video Call basi achana na huyo mtu! Narudia achana na huyo mtu na acha mazoea kabisa kwani ni suala la muda tu utaachwa na mume au mpenzi wako! Naomba nirudie, achana na huyo rafiki, huyo mwanaume si rafiki yako ni mchepuko wako!
Najua hajawahi kukutongoza, kukutamani, hajawahi kukuvunjia heshima ila ninakuambia kuwa kama imefikia hatua ya Video Call basi huyo mwanaume anakaribia kuvunjia ndoa yako. Kama unachart naye zaidi ya lisaa lizima basi ni suala la mdua tu utaachwa na ukishaachwa nina uhakika asilimia mia, kama hutaenda kumlilia akatembea na wewe kisha akakuacha basi akishasikia umeachwa naye atakatisha urafiki na wewe.
Kwa MABAHARIA wenzangu, kama mke au mpenzi wako anafanya huu upuuzi kwanza muambie aache mara ya kwanza, kisha mkumbushe muambie huo ushoga na wanaume kuchart umbea hutaki, akirudia tena siku moja mchukue, mpeleke kwa jamaa, kisha mauche huko na muambie waendelee kuchart mpaka wakichoka ndiyo arudi. Acha kuruhudu mke au mpenzi wako kufanya huu upuuzi kwani huyo jamaa siku ukikorofishana na mke wako kidogo tu basi akimuegemea bega ushaibiwa! Narudia usikubali mke au mpenzi wako kuwa na rafiki ambaye wanapigiana Video Call au wanatumiana meseji masaa mawili kana kwamba wanamchamba mtu, utaibiwa!
Nasubiri ambao watasoma hapa na hawataacha na itakula kwao




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz