‘Chachandu’ na maana yake katika ulimwengu wa mahaba - EDUSPORTSTZ

Latest

‘Chachandu’ na maana yake katika ulimwengu wa mahaba


Wanaume wengi wa Kiafrika wanapenda sana mwanamke kuwa na chachandu kwani wanakwambia zinawapa raha na utulivu wanapokuwa faragha.
Wanapata vipi? Wanajua wao, lakini baada ya mada hii kufika tamati najua nitapata ujumbe mwingi ukieleza jinsi gani wanafurahika.
Leo ni wengi wanataka kujua zinavaliwa wakati gani, shosti si kila sehemu unavaa chachandu angalia na sehemu ya kuzivaa kwa sababu ukizivaa eneo la kazi utatafsiriwa vibaya, zile zinafaa kuvaliwa chumbani ukiwa na mpenzi wako tu.
Unajua zile zinatungwa na uzi huenda ukazivaa na ikatokea zikakatika hivi utajisikiaje ukiwa sokoni halafu zikakatika lazima utaona aibu na wengine hudiriki kuziacha hapohapo.
Cha kufanya shosti yangu vaa kwa raha zako wakati unahisi mumeo anataka kurudi nyumbani, ukishaoga na umeshajiandaa kwa kumpokea mume unaweza kuvaa chachandu kwani zitachangia kumuweka tayari mumeo.
Sasa basi zifahamu hasa maana za rangi ya chachandu hizi na kazi yake.
Ukiachia mbali kunakshi kiuno chako pia zinamaana kwa rangi mojamoja ingawa siku hizi wanawake wamekuwa wakichanganya rangi kwa ajili ya mapambo tu na kumvutia mume lakini kuna rangi ambazo ni viashirio vya lugha ya kuwasiliana na mwenzako pale utakapotaka abaini jambo fulani na maana hizi ndiyo nakuletea shoga yangu.
Rangi kama pinki, bluu, dhahabu hizi rangi hazina maana kwenye sita kwa sita ni urembo tu kupendezesha kiuno, hukatazwi kuzivaa shosti sasa ninazokufundisha ni hizi.
Nyekundu:  Ukimkuta mwanamke amevaa chachandu ya rangi hii unatakiwa kuelewa kwamba mwanamke huyu yupo kwenye hedhi, kwahiyo wewe fanya mengine lakini siyo safari ya kupeana maraha kwani kwa kufanya hivyo kiafya si vizuri unatakiwa kuwa mpole tu.
Nyeupe:  Ukimkuta mwanamke amevaa chachandu nyeupe hii humaanisha hana tatizo lolote litakalomfanya asikupe raha ya sita kwa sita, kwa hiyo ukitaka tu muda wowote unapata kwani anakuwa amejipanga kwa lolote.
Nyeusi: Ukimkuta mwanamke amevaa rangi hiyo, humaanisha ya kwamba yupo tayari kukupa raha za sita kwa sita lakini uwanja wake haujakatwa majani, kwa hiyo chaguo ni lako kama unataka kutumia siku nzima kutafuta goli haya, ama kama utamsaidia kumkatia majani uwanjani vizuri zaidi ama kama huwezi yote basi mpe muda akate mwenyewe.
Wanawake wa zamani walikuwa hawavai chachandu, wanatandika sita kwa sita vizuri kisha wanatupia langi wanayoona inamfaa kwa siku hiyo, baba akitoka safari anakuta chachandu ya rangi nyekundu iko kitandani anajua mkewe alikuwa anatumikia siku zake siku zinaenda.
Mashosti kuna wengine hawapendi kuvaa kabisa unaweza kutumia kwa kuitupia ile unayoona inakufaa kumfikishia ujumbe mume wako kwa siku hiyo, lakini kumbuka kwa kuivaa inaleta hamasa fulani na kukusaidia kumuweka karibu mumeo.
GPL




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz